LEKIDEA FOCUS OVERVIEW

LEKIDEA
is a registered Non-profit Organization of Kirua Vunjo East Moshi, by Natives from related Villages (Kileuo, Mrumeni, Kotule, Mero, Legho, Lasso, Kwa-Laria(Kanji), dedicated to join together, leverage their Vision, Objectives, Social strengths, ambitions & professionalism and other common resources from members, relatives and families having any origination with K.V East, to come TOGETHER, DEVELOP and CHANGE their Motherland through Projects and involvements in different Social development Initiatives that play roles in alleviating poverty and enhancing opportunities in collaboration with all well wishers, and support from social development entities from the village level, national level, and international level.

LEKIDEA :: Miradi Mikuu; Barabara Uchira-Kisomachi

MRADI MKUU WA BARABARA YETU;

LEKIDEA IMEWEKA KIPAOMBELE KIKUU KATIKA UKARABATI WA BARABARA YETU KUU YA KUANZIA UCHIRA - KARUMELI HADI JUU KWA-LARIA (KANJI),  NA MRADI HUU UNAJUMUISHA PIA BARABARA NDOGO ZINAZOTOKA VIJIJINI NA VITONGOJI VYOTE MUHIMU IFUATAVYO, KISOMACHI - HADI LEGHO (KNCU) KUPITIA KISANJA, KISOMACHI HADI KWA-RENE (SUMI) KUPITIA KNCU, KNCU HADI KILASANIONI KUPITIA USANGI, KITAARINI HADI LASSO-KIWELEWELE KUPITIA KWA-MATAY, MANZAONI, KAMA BAADHI YAKE ZINAVYOONYESHWA KATIKA RAMANI ILIYO CHINI.

MRADI HUU WA UKARABATI WA BARABARA ZETU NI SEHEMU YA MIRADI MINGINEYO MINGI AMBAYO LEKIDEA KAMA TAASISI YETU RASMI IMEIWEKA MEZANI TAYARI KWA AJILI YA UHAMASISHAJI NA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA HARAKA NA WA UFANISI.

RAMANI HII INAONYESHA PICHA YA JUMLA YA MRADI WENYEWE NA UPANA WAKE, AMBAPO NGUVU, JUHUDI NA USHIRIKIANO WA KILA MWANA-KIRUA VUNJO MASHARIKI, TAASISI NA IDARA ZA KUJAMII NA KISERIKALI ZA KIKANDA ZITAHUSISHWA.






Kama ilivyoonyeshwa katika Ramani juu, Mradi huu ndio muhimu sana kwa Ufanisi, kuondoa Umaskini na udhaifu wa Jamii yetu yote inayotegemea sana Barabara ya Uchira hadi Karumeli hadi Kwa-Laria (Kanji). Pia Mradi huu utajumuisha Njia zitokazo katika Vijiji na Vitongoji Muhimu vya Ukanda wetu, ikiwa ni pamoja na Legho, Lasso, Kwa-Laria, Mero, Usangi, Manzaoni, Kileuo, Kotule, Mrumeni na Kileuo Kati.

LEKIDEA imeweka Mikakati ya Kuhusisha wanajamii wa Kada zote katika shughuli nzima za Ukarabati na Usafishaji wa Njia na Barabara hizi, ikiwa ni pamoja na Wananchi wa Vijiji tajwa kuandaa Siku rasmi za Nguvu-Kazi au Harambee (ilijulikana awali kama 'Jumatatu'), na hii itajumuisha Uongozi kwa ngazi za Mitaa, Vijiji na Kata, na pia Wenyeviti wa Kada zote hizo pamoja na Diwani wetu Mh. Alex Umbella; watakuwa ndio Mihimili mikuu ya Usimamiaji kazi na utekelezaji.

Kadhalika LEKIDEA imeweka lengo kushirikisha Taasisi zote za Kijamii ikiwa ni pamoja na Makanisa wa Makanisa yote, Karumeli na Legho, na pia mengineyo madogo-madogo, katika kuhamasisha Wanajamii wote walio katika Ukanda wetu kujituma, kuwajibika na kuendeleza juhudi la LEKIDEA za ukombozi wa eneo letu.

LEKIDEA imekusudia kuwa Mstari wa mbele katika Kushirikiana na Halmashauri na Kamati Tendaji, na pia Mfuko wa Jimbo la Vunjo, unaosimamiwa na Mbunge wetu, Mh. Augustine Lyatonga Mrema, ili kuhakikisha kuwa kila senti iliyotengwa kwa ajili ya maendeleo ya Ukanda wetu inapatikana, na inasimamiwa vyema ipasavyo katika kukamilisha miradi yetu yote, tukianzia na huu mradi mkuu wa Barabara zetu.

 JAMBO LA MUHIMU NI UHAMASISHAJI, TUUNGANE WOTE, TUSHIRIKIANE WOTE, TUCHANGIE MENDELEO HAYA ILI TUJIKOMBOE, TUONDOKANE NA AIBU YA MIAKA YOTE YA 'KUWA NYUMA' KULINGANA NA KANDA NYINGINE ZA MKOA WA KILIMANJARO, MKOA ULIOPEWA NEEMA NA KUJULIKANA DUNIA NZIMA, BALI SISI TUNAJIDHARAU NA KUSAHAU UMUHIMU WETU NA ENEO LETU.

TUKIANZA VYEMA, TUKIHAMASHISHANA WOTE NA KUENDELEA MBELE, WENGINE WATAIGA NA WATATUUNGA MKONO. TUSHIRIKIANE KATIKA MRADI HUU WA BARABARA ZETU, NA HESHIMA ILIYOPOTEA ITARUDI MUDA SI MREFU:

Hali kama inavyoonekana juu ndio imekuwa hali halisi katika barabara zetu na hivyo kuondoa hata ile thamani kubwa ya Ukanda wetu kikanda, kiwilaya, kimkoa na hata kitaifa. Hii yafaa kuondolewa mapema, na ndiyo lengo la LEKIDEA
Hali ya Barabara inapokuwa dhaifu, hata usafiri huwa dhaifu, wa hofu na wa kukatisha tamaa, na hili ndilo tunalokabiliana nalo kama inavyoonekana juu, Wananchi wasafiri wanakwama na kuchelewa kufika katika maeneo yao ya kiutendaji kutokana na Barabara kutokuwa za uhakika na kuaminika, kama ilivyo katika Ukanda wetu. LEKIDEA inakusudia kuhakikisha kuwa hali kama hii imebaki kuwa historia.

LEKIDEA imekusudia kuweka mikakati kwa Barabara zetu hasa Uchira - Karumeli hadi kwa Laria kuwa za kupitika muda wote bila kujali msimu wa mvua au jua. Barabara kama hii inapotengenezwa vyema na mfumo wa maji kuainishwa vyema, inaweza kupitika misimu yote, na kwa kada zote, yaani wapita kwa miguu na wenye magari. Kinachotakiwa ni usimamizi.
Juhudi zinapoonekana kuwa za Uhakika na maendeleo kuanza kuonekana, inakuwa rahisi kwa Taasisi muhimu zinazohusika na maendeleo, mfano Halmashauri na pia ngazi ya Wilaya na Mikoa, au hata taasisi na watu binafsi kutoa misaada ya vifaa kama Magreda ya usawazishaji na usambazaji, au uchimbaji wa mitaro kama inavyoonekana juu. LEKIDEA imekusudia kuunganisha nguvu za wananchi na Taasisi hizi muhimu ili kuhakikisha maendeleo yetu yanakuja.

Kaika kuharakisha mafanikio, LEKIDEA imeweka mikakati pia katika kuunganisha juhudi za wananchi na Taasisi muhimu za maendeleo za kikanda, kiwilaya na kimkoa katika kuhakikisha kuwa pale Barabara zetu zinapokarabatiwa kwa uhakika, usambazaji wa Moram kwa kiwango bora unakamilishwa ili kudumisha uimara wa Barabara husika. LEKIDEA imekusudia pia kusimamia suala la upatikanaji wa Moram wa kutosha katika kukarabati Barabara yetu ya Uchira-Karumeli hadi Kwa-Laria, ambao mwingi unapatikana katika eneo la ukanda wetu ambapo pia karibu kabisa na maeneo ya utekelezaji.
 
Barabara yetu inapokarabatiwa na kukamilika kwa kiwango kama hiki, inakuwa rahisi zaidi kusimamia ukarabati wa msimu (maintenance), hasa kuhusu suala la kunyoosha mifereji ya maji na kuzibua mitaro na makalvati ya nayoziba pale mvua kubwa zinaponyesha au mara nyingine watu wasio waangalifu wanapotupa takataka-ngumu ambazo huziba na kuzuia maji kupenya. LEKIDEA imekusudia barabara kama hii iwewepo hadi katika ngazi ya Vitongoji vyetu.

Barabara iliyotengenezwa na kukarabatiwa vyema, na kuwekwa Moram uliochanganywa vyema na kushindiliwa ipasavyo huinekana kuwa Imara, hudumu na kupitika katika wakati wote wa mwaka na hivyo huvuta hata wawekezaji wadogo-wadogo na wa kati, mfano watoaji wa huduma za usafiri, biashara na huduma za jamii, mfano mashule na taasisi nyinginezo kuhamasika na kuvutiwa na uhakika wa Barabara na hivyo kuharakisha uwekezaji, na kukuza maendeleo. Ukanda wetu umerudi nyuma kutokana na kukosa Barabara za uhakika na hivyo kufanya hata fursa za Biashara ndogondogo kwa wananchi wetu kuwa ngumu. LEKIDEA imeweka kipaombele kuhusu kukamilishwa kwa Barabara za Ukanda wetu kwa kiwango cha Moram ulioshindiliwa vyema na imara kama inavyoonekana juu ili kuimarisha maisha na uhakika wa biashara, vitega uchumi na maendeleo ya wananchi wa vijiji na vitongoji vyetu kule tulipotoka.




LENGO KUU NA MUHIMU, TUSHIRIKIANE, TUUNGANE NA TUCHANGIE MAENDELEO HAYA MUHIMU KWETU NA KWA VIZAZI VIJAVYO NA TUNAYOYAFANYA LEO YATAKUWA KUMBUKUMBU KUU NA HISTORIA YETU NA VIZAZI VYETU VYOTE.

______________&&&&___________


MIRADI MINGINEYO

LEKIDEA IMEWEKA PIA MIKAKATI KAMILI KATIKA MIRADI MINGINEYO MBALIMBALI KWA AJILI YA JAMII NZIMA IKIWEPO MAENDELEO YA VIJANA NA WANAWAKE NA HARAKATI ZA UHAMASISHAJI NA USHIRIKIANO IKIJUISHA TAASISI MUHIMU ZA KIJAMII NA ZA KISERIKALI IPO MEZANI KWA AJILI YA UTEKELEZAJI MAPEMA IWEZEKANAVYO, HASA MARA YA BAADA YA MRADI HUU MUHIMU WA BARABARA KUSONGA MBELE, MAANA NDIO UTAKAOFUNGUA NJIA NA NAFASI KWA WANANCHI WETU KUFAIDI MAENDELEO NA BIASHARA ZA NDANI NA NJE YA UKANDA WETU.

MIRADI MINGINE IMEAINISHWA KATIKA MTIZAMO WA PICHA NA MAELEZO KATIKA KURASA ZILIZOPO KATIKA MTANDAO HUU WA LEKIDEA. WOTE TUNAOMBWA KUPITIA KURASA HIZO KWA UTULIVU NA KUCHAMBUA MIRADI ILIYOAINISHWA, ILI KUTOA USHAURI, MAPENDEKEZO NA MIKAKATI ZAIDI YA KIUTEKELEZAJI, NA YOTE HAYO YATAPOKELEWA NA KUFANYIWA KAZI LA UONGOZI WA LEKIDEA.

________________&&&&_______________

TUPO PAMOJA, TUSHIRIKIANE, TUTAFIKA HARAKA!
--________________&&&&_______________
--