LEKIDEA FOCUS OVERVIEW

LEKIDEA
is a registered Non-profit Organization of Kirua Vunjo East Moshi, by Natives from related Villages (Kileuo, Mrumeni, Kotule, Mero, Legho, Lasso, Kwa-Laria(Kanji), dedicated to join together, leverage their Vision, Objectives, Social strengths, ambitions & professionalism and other common resources from members, relatives and families having any origination with K.V East, to come TOGETHER, DEVELOP and CHANGE their Motherland through Projects and involvements in different Social development Initiatives that play roles in alleviating poverty and enhancing opportunities in collaboration with all well wishers, and support from social development entities from the village level, national level, and international level.

Sunday, August 5, 2012

KIKAO CHA LEKIDEA 22-07-2012 NA TAARIFA RASMI

Wapendwa Wana-LEKIDEA, na Wapenda Maendeleo wote wazaliwa wa Ukanda wa Legho-Kirua Vunjo Mashariki, na Wapenda maendeleo wote popote walipo Tanzania na Dunia Nzima. Salaam ziwafikie!

Uongozi wa Taasisi yetu muhimu ya Legho-Kirua Develeopment Association (LEKIDEA), hivi karibuni (22/07/2012) ulifanya Kikao Muhimu cha kufuatilia mambo muhimu na Utekelezaji wa Miradi iliyo katika Mikakati na Malengo ya Taasisi hii muhimu inayolenga kunyanyua maisha ya Eneo walilozaliwa la Legho-Kirua Vunjo Mashariki. Kikao kilikuwa cha manufaa sana.

Pamoja na Mambo mengine muhimu, Kikao hiki kilichoongozwa na M/Kiti wa Taasisi Ndg Edward F. Msaky, kilikuwa cha mafanikio makubwa, na kiliweza kujenga midani na mikakati bora kabisa katika kuifanya Taasisi kutimiza malengo yake na majukumu muhimu iliyojiwekea katika kuukomboa ukanda wetu katika hali ya 'kusahaulika' kimaendeleo na kiuchumi. Baadhai ya masuala muhimu yaliyofanyiwa kazi ni pamoja na Kufuatilia kwa umakini Mradi wa Ukarabati wa Barabara za Vijiji vyote vya Legho-Kirua Vunjo, (kama ilivyoainishwa katika Taarifa Rasmi kwa Vyombo vya Habari 'Press Release' chini) ambapo Mradi wenyewe ulishaanza. 

Pia mikakati mingine katika Kikao ilihusu uhamasishaji zaidi wa wazaliwa wote wa maeneo ya Legho-Kirua Vunjo Mashariki popote walipo ili waweze kuungana zaidi na kuchangia kwa hali na mali katika kuhakikisha maendeleo yaliyokusudiwa kwa kupitia taasisi hii ya LEKIDEA inafanikiwa kwa kiwango kikubwa ili kufaidisha wananchi wote wa sasa na vizazi vijavyo. 

Kadhalika, suala muhimu la kuwafahamisha wanachama wote wa Legho-Kirua, Tanzania nzima na wapenda maendeleo wote, hali halisi na maendeleo ya Michango ya wanachama, Miradi na malengo ambayo yalikwishafikiwa hadi sasa, ili kwa njia moja au nyingine waendelee kuhamasishana kila mwanachama na kuutambua umuhimu wa kuunga mkono juhudi hizi za LEKIDEA, kadhalika na taasisi za ndani na nje ya nchi ambazo zinathamini hatua na juhudi hizi za maendeleo kwa ngazi ya chini (vijijini) zinazofanywa na LEKIDEA, na juhudi zilizokwishafanyika hadi sasa, wapate kutuunga mkono na kuchangia maendeleo yetu kwa hali na mali kwa kupitia Taasisi yetu hii Rasmi iliyosajiliwa kwa malengo na dhamira ya kuukomboa ukanda wetu kiuchumi, kijamii na yote yanayohusika nayo. Dalili ni njema sana na yafaa kutuunga mkono, na haraka tutasonga mbele zaidi.

Chini hapa ni baadhi ya Picha za matukio kadhaa muhimu zitokanazo na Kikao hicho:

Kutoka kushoto: Mwenyekiti wa LEKIDEA, Ndg Edward Msaky, akipitia kwa umakini taarifa na oradha ya mambo muhimu yaliyokuwa yakijadiliwa katika kikao. Katikati ni Katibu wa LEKIDEA Ndg Joseph Shewiyo akifafanua agenda kwa Wajumbe, na kulia kwake ni Makamu M/Kiti Eng. Simon Njau, akipitia baadhi ya majina ya Wanachama katika Simu yake katika kuwasiliana nao yale yanayoendelea katika kikao.

Kutoka kushoto: Mjumbe wa Kikao Mh. Adocate Minja, na katikati ni Eng. Bernard Ndepachio Msacky, na kulia kwake ni Mwanasheria wa Taasisi, Wakili Tonny Teye, wakisikiliza kwa makini maendeleo ya agenda katika kikao.
Wajumbe wa Kikao cha LEKIDEA, kutoka kushoto; Ndg Emilian Saluo Assey, akifuatiwa na Ndg Venance V. Msacky, akifuatiwa na Ndg Amani-Ereney Beda Kyara na wa mwisho kulia ni Ndg Gabriel Kessy, wote wanaonekana wakifuatilia kwa makini agenda za kikao zilivyokuwa zikifafanulia.
Wajumbe wa Kikao cha LEKIDEA, kutoka kushoto; Ndg Paul Sanene Z Msaki, akifuatiwa na Ndg Martin Mathias Kessy, ambaye pia ni Makamu-Katibu wa LEKIDEA, na mwicho kulia ni Ndg Emilian Saluo Assey wakisikiliza kwa utulivu masuala muhimu ya utekelezaji kama yaliyokuwa yakielezwa toka meza kuu.
Katika picha juu, anaonekana Katibu Mkuu wa LEKIDEA Ndg Joseph Ignas Shewiyo anachambua vipengele muhimu kutoka katika agenda zinazojadiliwa na kulia kwake M/Kiti, Ngd Edward Msaky akifuatilia sambamba na Makamu-M/Kiti Eng. Simon Njau akiendelea kuwasiliana na baadhi ya wajumbe katika kufanikisha uchangiaji.
Pichani: Toka kushoto, Makamu Katibu wa LEKIDEA Ndg Martin Kessy akifuatiwa na Ndg Emilian Saluo Assey na kulia kwake ni Ndg Amani-Ereney Kyara, wote wakisikiza na kufuatilia maendeleo ya kikao.
Hiki ndicho kikosi kamili kilichoketi katika kikao hicho muhimu kwa masaa karibia manne bila kuchoka, na kufanuikisha majukumu na masuala muhimu sana ya kiutekelezaji ambayo ndiyo msingi wa LEKIDEA na jamii nzima kuendelea kusonga mbele. Ari, moyo wa kujitolea na umahiri wao katika kufuatilia utendaji ndio dira na nguvu ya LEKIDEA ambayo kila mmoja wetu na yeyote mpenda maendeleo yafaa kuunga mkono. Kuoka kushoto waliosimama: Ndg Venance V Msacky, Ndg Gabriel Kessy, Mh Advocate Minja, Ndg Paul Sanene Z. Msaki, Ndg Emilian Saluo Assey, Ndg Amani-Ereney Beda Kyara, Eng Bernard D. Ndepachio Msacky, na Ndg Tonny Teye. Waliokaa, kuanzia kushoto:  Ndg Martin Mathias Kessy, Ndg Edward F. Msaky, Ndg Joseph Ignas Shewiyo na Eng Simon T Njau. Mjumbe mmoja Ndg Sylvester A. Matemu (hayupo pichani) aliwahi kuondoka kutokana na majukumu ya dharuara yaliyomlazimu kuwahi kuondoka.
 -------------------&&&----------------------

WAPENDWA WANA-LEKIDEA, NA WANANCHI WOTE WENYE MAPENZI MEMA YA KIMAENDELEO, HII HAPA NDIYO TAARIFA RASMI YA LEKIDEA KAMA ILIVYOTOLEWA KATIKA GAZETI THE GUARDIAN LA TAREHE 03/08/2012.


MWANA-LEKIDEA, TUENDELEE KUCHANGIA MAENDELEO YETU PASIPO KIKWAZO, AU KUKATISHWA TAMAA NA MTU AU KIKUNDI CHOCHOTE, MAANA KUDHOOFU KWETU NDIO MTAJI KWA WENGINE, NA TUJITAMBUE DAIMA KUWA MAENDELEO YETU YATALETWA NA SISI WENYEWE, ....NA WAKATI NDIO SASA!! TUUNGANISHE NGUVU!