LEKIDEA FOCUS OVERVIEW

LEKIDEA
is a registered Non-profit Organization of Kirua Vunjo East Moshi, by Natives from related Villages (Kileuo, Mrumeni, Kotule, Mero, Legho, Lasso, Kwa-Laria(Kanji), dedicated to join together, leverage their Vision, Objectives, Social strengths, ambitions & professionalism and other common resources from members, relatives and families having any origination with K.V East, to come TOGETHER, DEVELOP and CHANGE their Motherland through Projects and involvements in different Social development Initiatives that play roles in alleviating poverty and enhancing opportunities in collaboration with all well wishers, and support from social development entities from the village level, national level, and international level.

Monday, December 10, 2012

LEKIDEA: KIKAO CHA TATHIMI YA MIRADI, DIRA 2013, UJUMBE WA M/KITI

IFUATAYO NI TAARIFA FUPI YA KIKAO CHA TATHMINI YA MIRADI, 2012, NA DIRA MPYA 2013.
-------------------------

KIKAO CHA LEKIDEA


KUTATHMINI MIRADI YA LEKIDEA
NA DIRA YA MWAKA MPYA 2013

Venue: DOUBLE VIEW HOTEL, SINZA – DSM.
Date: 02/12/2012

MINUTES ZA KIKAO

AGENDA

1. Writeups: Food Aid & JICA nk.
2. Media Conference na Statement kwa Wana-LEKIDEA na Umma wote.
3. Programme na Dira ya Mwaka Mpya 2013.
4. Ada ya Kila Mwana-LEKIDEA na Manufaa yake.
5. Mengineyo

MCHANGANUO WA AGENDA

Kufungua Kikao:
Kikao kilifunguliwa saa 12:00 jioni kwa sala.

1.      Writeups: Food Aid & JICA:
Ø  Kikao kiliafikiana kuwa Katibu, Ndg Joseph Shewiyo ataandaa Draft ya Writeups na kuiwasilisha kwa Sekretariat ambayo itaipitia, kuijadili na kuikamilisha mapema kwa ajili ya kusambaza ktk taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Food Aid na JICA ili kutafuta ufadhili wao kwa miradi ijayo ya LEKIDEA.

2.      Report ya Sekretariat kwa Wana-LEKIDEA na Umma
Ø  Sekretariat iliwasilisha taarifa kwa ufupi kuhusu mradi wa barabara ulivyokwisha kufikia hadi sasa, na malengo yajayo ili kuhakikisha kuwa tuna maendeleo endelevu.
Ø  Kikao kiliafiki kuwa iandaliwe Taarifa rasmi (Media Statement) ya jumla, itakayounganisha ile Taarifa kwa Umma iliyotoka awali pamoja na Taarifa mpya ya mwaka mpya itakayotoka hivi karibuni, ili iwasilishwe kwa vyombo vya Habari katika mipangilio ifuatayo:
ü  Katibu kuandaa makala ili itolewe kwenye vyombo vya habari.
ü  Iandaliwe Taarifa iliyokamilika vyema (Media Statement), ikionyesha Profile ya LEKIDEA na miradi yake na mafanikio hadi sasa.
ü  Taarifa hii pia itaunganisha taarifa ya awali iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari, pamoja na taarifa mpya ya Mwaka Mpya 2013, pamoja na picha za wananchi na Miradi ilivyokuwa inafanywa, na Video za kazi zilivyokuwa zikiendelea.
ü  Mh Diwani Alex Umbella aliahidi kuwasilisha video za matukio hayo ili ziweze kutumika ktk kuandaa Media Conference hiyo.
ü  Tukio hili litawasilishwa na M/Kiti, pamoja na Katibu au Kaimu Katibu, ktk Ukumbi wa HABARI MAELEZO, na maandalizi yanafanyika ili iweze kufanyika kabla ya Tarehe 15/12/2012.

3.      Programme Kubwa na Dira ya Mwaka Mpya 2013:
Ø  Kikao kiliafiki kuwa katika kuendeleza malengo ya mafanikio ya wananchi wetu, LEKIDEA imeainisha malengo na mipango kabambe kwa Mwaka Mpya 2013 kama ifuatavyo:
ü  Kumalizia ujenzi wa barabara kwa kujenga culverts na barabara ndogondogo za ndani, pia kuongezea moram sehemu zenye upungufu

ü  Kuanzisha vitalu vya miche ya miti hususan ya Mierezi (gravelia) ipatayo 10,000/- (elfu kumi) kwa kuanzia ambayo itatolewa kwa wanavijiji ili wapande katika maeneo mbalimbali ya ukanda wetu ikijumuisha kando ya barabara zetu, na ktk kingo za mashamba.
ü  Mhe Diwani atafuatilia ufufuaji na uendelezaji wa bwawa la Urenga kwa kuhimiza Halmashauri ya Wilaya ilifufue na kuliendeleza kwa ajili ya umwagiliaji.  Hili litawezesha wananchi wetu kufaidika na Samaki, na umwagiliaji wa Mboga na mazao mengineyo.
ü  Harambee ya kuchangisha hela za maendeleo ya miradi ya Lekidea  kufanyika ndani ya Februari 2013 ili kuwahi mvua za Masika kwa ajili ya Moram, Maintenance ya Njia na Coverts nk.

4.      Ada ya Kila Mwana-LEKIDEA
Ø  Kikao kiliafiki kuwa ili kuwezesha taasisi yetu iweze kusonga mbele kwa mafanikio na kuwatumikia wananchi pasipo kukwama popote, kila mwana-LEKIDEA na mpenda-maendeleo atatoa ada ya kudumu ya Sh 100,000/- (Laki moja) kwa mwaka, ada ambayo itakuwa nyezo kwa LEKIDEA na Malengo yake ya muda mrefu LEGHO-KIRUA ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa yafuatayo:-
ü  Lengo kuu; Kuendeleza, Kusimamia (Maitenance) Barabara zetu zote kwa kipindi chote cha mwaka mzima.
ü  Lengo jingine; Ada hii pia itatumika kama sehemu ya uchangiaji wa masuala ya maendeleo endelevu ya Legho-Kirua na hivyo LEKIDEA itatambua na kuthamini sana nafasi na kipaumbele cha mchangiaji katika kushirikiana naye masuala ya kijamii.
ü  Manufaa kwa Mtoa Ada: Kutokana na umuhimu wa kuwezesha maendeleo yetu kuwa endelevu, LEKIDEA itamtambua na kumthamini kila mtoa ada ya uanachama kwa kuhamasisha wengine kushirikiana naye katika masuala muhimu ya kijamii atakayokabiliana ikiwa ni pamoja na matukio kama Misiba, Harusi, Magonjwa nk.
ü  Madhara ya Kutokutoa ada; Wapo wazaliwa wa Legho-Kirua ambao mbali na kusikia, kuhamasishwa na kusukumwa sana kuchangia maendeleo na miradi yetu, wamekuwa wagumu sana, wengine wakibeza, na kudharau juhudi hizi, na pia wengine kuwakwaza wengine ili tu kuwakatisha tamaa wasichangie umoja huu. Huu ni mwenendo usiokubalika.
ü  Hivyo basi, kulingana na umuhimu wa ada hii kwa maendeleo ya jamii yetu, mwananchi atakayekwamisha au kushindwa kuunga mkono na kutoa ada hii kwa malengo yasiyo dhahiri, au kwa visingizio visivyoeleweka, wakati ukweli ni kuwa, ameshafaidika na anafaidika kwa sasa na ataendelea kufaidika na jasho la wengine wapenda maendeleo wa Legho-Kirua waliokwisha kuchangia kwa hali na mali, taasisi ya LEKIDEA haitamvumilia mtu wa mwenendo huo, na haitasita kumfichua, na pia kuwafahamisha wanachama na wananchi wote wapenda maendeleo wa Legho-Kirua ili watambue mwenendo wa mtu husika, na hata ikiwezekana, LEKIDEA itachukua jukumu la kwanza kuhamasisha pale inapowezekana ili mwananchi kama huyo asiweze kuungwa mkono, au kuchangiwa katika masuala ya kijamii kama misiba, harusi, magonjwa nk. ‘Asiyeotesha nawe hawezi kuvuna nawe’

5.      Mengineyo
Ø  Lobbying: Kikao kilipendekeza uwepo mpango wa kukutana na Engineer wa Manispaa kwa Mazungumzo ya Maendeleo yetu, hasa kuhusu budgets allocation, hasa ktk mifereji ya maji ambayo ni kati ya chaguo letu kubwa ktk maeneo ya utekelezaji.

Kikao kilifungwa saa 3:45 usiku kwa sala.

HAHUDHURIO:
1.       Eng Simon T Njau - Makamu/MKti
2.       Joseph I Shewiyo - Katibu
3.       Martin M Kessy - Makamu/Katibu
4.       Mh Alex Umbella - Diwani wetu
5.       Emilia J Saluo - Mwanasekretariat
6.       Paul Z Msaki - Mwanasekretariat
7.       Stephen Vendelin Msacky - Mjumbe
8.       Dr Kessy, Mkoloni - Mjumbe

UDHURU:
1.       Edward F Msaky - M/Kiti
2.       Eng Bernard D. Ndepachio - Mwanasekretariat.
3.       Aman Beda Kyara
4.       Venance Vendelin Msacky



--------------------                                               ----------------------
Katibu                                                                                M/Kiti

Katika kuwakumbusha Wana-LEKIDEA katika kutoa michango yao, wasisite kutumia njia zifuatazo:
AKAUNTI YA LEKIDEA:        Bank: CRDB BANK Plc.:
Jina la A/C:   LEGHO KIRUA DEVELOPMENT ASSOCIATION
A/C No:   0152095786500
SIMU MKONONI ZA LEKIDEA:       
§  Vodacom – MPESA:  0755 799 133
§  Tigo – TigoPESA: 0653 799 133
MWISHO


-------------------------&&&&&---------------------------

HABARI ZA MAENDELEO YA KIRUA VUNJO MASHARIKI CHINI YA USIMAMIZI WA LEKIDEA KAMA ZILIVYORIPOTIWA NA MAGAZETI YA THE GUARDIAN NA NIASHE HIVI KARIBUNI.
 ---------------------------

UJUMBE NA SALAMU RASMI ZA MWENYEKITI WA LEKIDEA KWA AJILI YA X-MASS 2012 NA MWAKA MPYA 2013 KWA WATU WOTE