LEKIDEA FOCUS OVERVIEW

LEKIDEA
is a registered Non-profit Organization of Kirua Vunjo East Moshi, by Natives from related Villages (Kileuo, Mrumeni, Kotule, Mero, Legho, Lasso, Kwa-Laria(Kanji), dedicated to join together, leverage their Vision, Objectives, Social strengths, ambitions & professionalism and other common resources from members, relatives and families having any origination with K.V East, to come TOGETHER, DEVELOP and CHANGE their Motherland through Projects and involvements in different Social development Initiatives that play roles in alleviating poverty and enhancing opportunities in collaboration with all well wishers, and support from social development entities from the village level, national level, and international level.

Friday, March 23, 2012

LEKIDEA: MRADI WA BARABARA ZA VIJIJI - AWAMU YA 1:

Ndugu wana-LEKIDEA

Tunawasalimu wote tena kwa Jina la Mwenyezi na tunawapa pole kwa majukumu mengi ya mwaka mpya.
Kama mjiavyo, Sekretariet imekuwa inafanya kazi juu chini kuhakikisha kuwa jambo muhimu tulilolianza linatekelezwa kama inavyotakiwa.
Awali tulitegemea hatua za Halmashuri yetu lakini baada ya kuona kuwa zinachelewa Sekretariat imeandaa 'mpango-kazi' wa utekelezaji kwa barabara zetu za, kule juu kuanzia Kisomachi kwenda Vijijini. Wote tuelewe kuwa kwa kuwa hatuna mamlaka ya kutengeneza barabara ya Uchira-Kisomachi bila kupitia Halmashauri, ndiyo maana hatujaiweka katika mpango huu wa awamu hii ya sasa.
Halmashuri itakapoanza ujenzi sisi bado tutaingia humo kama tulivyoahidi na kufafanua katika mpango wa kwanza. Kwa sasa tunapendekeza utekelezaji uwe kwa LEKIDEA kukubaliana na Mkandarasi wetu kuanza ujenzi wa barabara za vijiji zifuatazo zenye jumla ya kilomita 12 (tazama barabara nyekundu kwenye ramani iliyoambatanishwa chini).

BARABARA HUSIKA - AWAMU YA 1:
- Kisomachi hadi Kwa-Laria kupitia Mero Kati
- Kwa-Matay hadi Laso juu (Mkombenyi) kupitia Manzaoni-CCM na Kiwelewele
- Kisomachi hadi Kapero Center
- Kisomachi hadi Shule ya Kilimani kupitia Mrumeni
- Kitaarini hadi KNCU


Ndugu wana LEKIDEA wote, kama mnavyoona kwenye jedwali la gharama tunaweza kuanza ujenzi kwa hatua (1) (ktk Jedwali), ambayo ni kujenga mitaro ya maji na culverts, Ili tuweze kuendelea na kuchonga barabara hizo (grading) namba (2), kwa kiwango stahiki tutahitaji kubanana sana walikwishatoa pledge tunawaomba wakamilishe na ambao bado wote tuungane watoe michango yao, na wote tuhimizane kwa nguzu zote. 
Nia yetu ni kukamilisha hadi namba (3) ksms inavyoonyeshwa katika Jedwali, ambayo ni Moram na compaction ni gharama kubwa lakini tunataka kila mtu ajitoe hasa wale wengi ambao bado. Kadahalika tumewaomba wazazi waliopo katika Vijiji vyote, wahimize watoto wao na wao wenyewe washiriki.
Tunatafuta ushauri wa wataalamu kuhusu mvua za masika kama ni busara kuanza kabla au baada ya mvua. Hata hivyo utekelezaji ni lazima, tumeanza lazima tufike. Sasa tunaomba maoni yenu katika vipengele vyote ikiwa ni pamoja na namna ya kupata fedha ya kutosha kukamilisha kazi hiyo muhimu katika hatua hii tunayotaka kuchukua sasa.
Tunawategemea sana Ngd Wafuatao katika kufuatilia na kutoa Mwongozo na Uangalizi katika mradi huu muhimu: Eng Bernard D. Msacky, Eng. Simon Njau, Eng.Bona na tunatangulia kuwashukuru WOTE kwa kufanya kazi hii endelevu na iweze kufanikiwa vyema. 
Tunawaomba wote kutoa maoni na mawazo endelevu mapema NDANI YA WIKI MOJA, ili kufikia muafaka ma kuwezesha mradi huu kuanza.
PAMOJA DAIMA, TUTAFANIKIWA HARAKA.

TYK......,
SEKRETARIAT - LEKIDEA,
 ------------------------------------------------------------------------------------------

RAMANI YA BARABARA HUSIKA KATIKA AWAMU HII:

MAKISIO YA GHARAMA KWA AWAMU HII YA 1